unfoldingWord 43 - Kanisa Linaanza

unfoldingWord 43 - Kanisa Linaanza

Outline: Acts 1:12-14; 2

Script Number: 1243

Language: Swahili

Audience: General

Genre: Bible Stories & Teac

Purpose: Evangelism; Teaching

Bible Quotation: Paraphrase

Status: Approved

Scripts are basic guidelines for translation and recording into other languages. They should be adapted as necessary to make them understandable and relevant for each different culture and language. Some terms and concepts used may need more explanation or even be replaced or omitted completely.

Script Text

Baada ya Yesu kurudi mbinguni, wanafunzi wake walibaki Yerusalem kama alivyowaagiza kufanya. Waumini wake walikuwa na utaratibu wa kukusanyika na kuomba pamoja.

Kila mwaka baada ya siku 50 za Pasaka, Wayahudi walisheherekea siku muhimu ya Pentekosti. Pentekosti ni kipindi ambacho wayahudi walisheherekea mavuno ya ngano, Wayahudi walikwenda Yerusalemu wakitokea ulimwenguni kote kusheherekea kwa pamoja Pentekosti. Mwaka huu kipindi cha Pentekosti kilikuwa baada ya wiki moja Yesu aliporudi mbinguni.

Wakati waumini wakiwa pamoja, ghafla nyumba ilijawa na sauti kama upepo mkali. Kisha kitu kama mwali wa moto kikaonekana juu ya vichwa vya waumini wote. Wote walijazwa na Roho Mtakatifu na kuanza kunena kwa lugha nyingine.

Watu wa Yerusalemu waliposikia kelele, kusanyiko la watu walikuja kushuhudia kilichotokea. Watu waliposikia waumini wakitangaza matendo ya ajabu ya kazi za Mungu, walishangaa sana kwa kuwa walisikia maneno hayo kwa lugha zao za asili.

Baadhi ya watu wakawashutumu wanafunzi kuwa wamelewa, lakini Petro akasimama akawaambia, nisikilizeni, hawa watu hawajalewa, bali unatimizwa unabii uliotolewa na Yoeli ambao Mungu alisema "Siku za mwisho nitamdhihirisha Roho"

Wanaume wa Israeli Yesu alikuwa mwanadamu alitenda miujiza na maajabu mengi kwa uwezo wa Mungu, nanyi mnajua na kuona lakini mlimsulubisha.

Ingawa Yesu alikufa, Mungu alimfufua kutoka kwa wafu na hii inatimiza unabii unaosema "Hutamwacha mtakatifu wako kuoza kaburini" Nasi tu mashahidi wa mambo hayo kuwa ukweli kwamba Mungu alimfufua Yesu.

Yesu anatukuzwa kwenye mkono wa kuume wa Mungu baba, na Yesu amemtuma Roho Mtakatiifu kama alivyoahidi kuwa angefanya. Roho Mtakatifu anasababisha mambo mnayoyaona na kuyasikia.

"Mlimsulubisha mtu huyu Yesu. Lakini mfahamu kwa uhakika Mungu amesababisha Yesukufanyika kuwa Bwana na Masihi.

Watu waliomsikiliza Petro walivutwa kwa undani na mafundisho aliyosema. Wakamwuliza Petro na wanafunzi. Je mnataka tufanye nini?

Petro akawajibu, "kila mtu anapaswa atubu na kubatizwa kwa Jina la Yesu Kristo na Mungu atawasamehe dhambi zenu. Kisha atawapa kipawa cha Roho Mtakatifu."

Yapata Watu 3,000 wakaamini alichokisema Petro wakawa wanafunzi wa Yesu. Nao wakabatizwa wakawa washirika wa kanisa la Yerusalemu.

Wanafunzi waliendelea kusikiliza mafundisho ya mitume, walikaa pamoja na kula pamoja na kuomba pamoja. Walifurahi wakamsifu Mungu kwa pamoja na walishirikishana kila kitu walichokuwa nacho kwa pamoja. Kila mtu alikuwa na mtizamo mzuri juu yao. kila siku watu wengi waliendelea kuamini.

Related information

Words of Life - Audio gospel messages in thousands of languages containing Bible based messages about salvation and Christian living.

Free downloads - Here you can find all the main GRN message scripts in several languages, plus pictures and other related materials, available for download.

The GRN Audio Library - Evangelistic and basic Bible teaching material appropriate to the people's need and culture in a variety of styles and formats.

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the right audio or video format - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?