unfoldingWord 29 - Simulizi ya Mtumishi Asiye na Huruma

unfoldingWord 29 - Simulizi ya Mtumishi Asiye na Huruma

Outline: Matthew 18:21-35

Script Number: 1229

Language: Swahili

Audience: General

Genre: Bible Stories & Teac

Purpose: Evangelism; Teaching

Bible Quotation: Paraphrase

Status: Approved

Scripts are basic guidelines for translation and recording into other languages. They should be adapted as necessary to make them understandable and relevant for each different culture and language. Some terms and concepts used may need more explanation or even be replaced or omitted completely.

Script Text

Siku moja, Petro alimuuliza Yesu "Bwana, ni mara ngapi inanipasa kumsamehe ndugu yangu akinikosea? Hadi mara saba?" Yesu akasema, "Sio mara saba, bali sabini mara saba!" Kwa hili, Yesu alimaanisha inatupasa kusamehe kila wakati. Yesu akawaambia habari hii.

Yesu akasema, " Ufalme wa Mungu unafananishwa na mfalme alie taka kukusanya madeni yake kutoka kwa watumishi wake. Mmoja wa watumishi wake alikua anadaiwa deni kubwa lenye thamani ya mshahara wa miaka 200,000."

Kwakua yule mtuishi hakuweza kulipa deni, mfalme alisema, 'muuzeni huyu mtu na familia yake kama watumwa ili kulipa deni lake.

Yule mtumishi alianguka na kupiga magoti mbele ya mfalme na kusema, ' naomba nivumilie, na nitalipa deni loote unalonidai.' Mfalme alimuonea huruma yule mtumishi, ndipo akafuta deni lake lote na kumuacha aende zake.

Ila baada ya mtumishi kutoka kwa mfalme, alimpata mtumishi mwenzake aliekua akimdai deni lenye thamani ya mshahara wa miezi minne. Alimkamata yule mtumishi mwenzake na kusema, ' Nilipe hela ninayo kudai!"'

"Yule mtumishi mwenzake alianguka na kupiga magoti na kumwambia, 'Tafadhali nivumilie, nitakulipa kiasi chote unachonidai.' Ila, yule mtumishi alimtupa mtumishi mwenzake ndani ya gereza hadi atakapo lipa deni lake.

Baadhi ya watumishi wengine walioona kilicho tokea walifadhaika sana. Wakaenda kwa mfalme na kumuambia kila kitu.

Mfalme alimwita yule mtumishi nakumuambia, 'Ewe mtumishi muovu! Nilikusamehe deni lako kwasababu ulinisihi. Ungefanya vivyo hivyo.' Mfalme alikasirika sana na kumtupa yule mtumishi muovu gerezani mpaka atakapo lipa deni lake lote.

Ndipo Yesu akasema " Hivi ndivyo baba yangu wa mbinguni atakavyo fanya kwa kila mmoja wenu kama hamtawasamehe ndugu zenu kutoka moyoni".

Related information

Words of Life - Audio gospel messages in thousands of languages containing Bible based messages about salvation and Christian living.

Free downloads - Here you can find all the main GRN message scripts in several languages, plus pictures and other related materials, available for download.

The GRN Audio Library - Evangelistic and basic Bible teaching material appropriate to the people's need and culture in a variety of styles and formats.

Choosing the audio or video format to download - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons