unfoldingWord 32 - Yesu Amponya Mwanamume Aliyepagawa - pepo na Mwanamke Mgojwa

unfoldingWord 32 - Yesu Amponya Mwanamume Aliyepagawa - pepo na Mwanamke Mgojwa

Outline: Matthew 8:28-34; 9:20-22; Mark 5; Luke 8:26-48

Script Number: 1232

Language: Swahili

Audience: General

Genre: Bible Stories & Teac

Purpose: Evangelism; Teaching

Bible Quotation: Paraphrase

Status: Approved

Scripts are basic guidelines for translation and recording into other languages. They should be adapted as necessary to make them understandable and relevant for each different culture and language. Some terms and concepts used may need more explanation or even be replaced or omitted completely.

Script Text

Siku moja Yesu na wanafunzi wake walipanda mashua kuelekea mjini, ambako waliishi watu wa Gerasini.

Na walipofika upande wa pili wa ziwa, na alikuwako mtu mwenye mapepo alimkimbilia Yesu.

Mtu huyu alikuwa mwenye nguvu na hapukuwa na mtu yeyote wa kumdhibiti. watu walimfunga kamba mikonom na miguuni mwake lakini bado aliweza kuzikata.

Mtu huyo aliishi maeneo ya makaburi na mtu huyu alitetemeka mchana na usiku kwa sababu hakuvaa nguo zozote na mwili wake alijikata kwa mawe.

Mtu huyo alipokuja kwa Yesu, alianguka mbele ya magoti yake. Na Yesu akaliaamuru lile pepo "limtoke mtu huyo".

Mtu huyo mwenye pepo akalia kwa sauti " unataka nini kwangu Yesu, mwana wa Mungu aliyetukuzwa juu? tafadhali usinitese" ndipo Yesu akaliuliza lile pepo " je unaitwa nani"? akajibu " jina langu ni legioni" na kwa sababu tupo wengi ( " legioni" kikundi cha wanajeshi maelfu katika vikosi vya rumi).

Yale mapepo yakamwomba Yesu " tafadhali usituondoe katika mji huu", na hapo palikuwa na kundi la nguruwe karibu na kilima, yale mapepo yakamwomba Yesu " tuamuru twende kwenye nguruwe hao" na Yesu akajibu "nendeni".

Yale mapepo yakamtoka yule mtu na kuwaingia wale nguruwe, Na wale nguruwe wakakimbilia huko chini bondeni kwenye ziwa........ na palikuwako na nguruwe 2000 kundini.

Na watu wale waliokuwa wakiwaangalia wale nguruwe walipoona hayo yakitokea, walikimbia na kuelekea mjini na huko wakamwambia kila mmoja yakuwa wamemkuta Yesu na aliyokuwa akitenda. Na watu wa mjini wakaenda na kumwona yule mtu aliekuwa na mapepo. Alikuwa amekaa kwa utulivu,amevaa nguo na alikuwa anaonekana kama mtu wa kawaida.

Watu waliogopa na wakamuomba Yesu aondoke, ndipo Yesu akapanda ndani ya mashua na akijiandaa kwa ajili ya kuondoka. na mtu yule aliekuwa na mapepo akamusihi Yesu aondoke pamoja naye.

Yesu akajibu " hapana, ondoka uende nyumbani na uwaeleze marafiki na familia yako kuhusu yote alivyokutendea Mungu na alivyokufanyia huruma yake kwako.

Ndipo mtu yule akaondoka na kumweleza kila mtu yale yote Yesu aliyomtendea. Na kila mtu aliye sikia simulizi hizi alishangaa na kusitaajabishwa.

Ndipo Yesu akarudi upande mwingine wa ziwa, na lipofika lilikuwako kundi kubwa la watu waliokusanyika wakimzunguka. na hapo alikuwapo mwanamke aliegua na kutokwa damu miaka kumi na miwili. Alilipa pesa yake yote kwa waganga ili wamponye lakini hali ilizidi kuwa ngumu.

Alisikia ya kuwa Yesu aliponya watu wengi na akafikiri" hakika kama nitagusa vazi la Yesu na mimi nitapona pia". hivyo akaja karibu na Yesu akamgusa vazi lake. na baada ya kumgusa tu, alipona na hakutokwa damu kwake kukaisha.

Na ndipo Yesu akagundua yakuwa nguvu zimemuishia, hivyo akageuka nyuma na kuuliza " je ni nani aliye nigusa", wanafunzi wakamjibu " kuna kundi kubwa la watu limekuzunguka na wakikugusa je ni kwa nini umeuliza "ni nani aliyenigusa"

Kisha yule mwanamke akaanguka magotini pa Yesu akitetemeka na kuogopa, akamwambia yale yote aliyo yatenda na alivyopokea uponyaji. Yesu akamwambia " enenda kwa amani, imani yako imekuponya.

Related information

Words of Life - Audio gospel messages in thousands of languages containing Bible based messages about salvation and Christian living.

Free downloads - Here you can find all the main GRN message scripts in several languages, plus pictures and other related materials, available for download.

The GRN Audio Library - Evangelistic and basic Bible teaching material appropriate to the people's need and culture in a variety of styles and formats.

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the right audio or video format - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?