unfoldingWord 42 - Yesu Anarudi Mbinguni

unfoldingWord 42 - Yesu Anarudi Mbinguni

Outline: Matthew 28:16-20; Mark 16:12-20; Luke 24:13-53; John 20:19-23; Acts 1:1-11

Script Number: 1242

Language: Swahili

Audience: General

Genre: Bible Stories & Teac

Purpose: Evangelism; Teaching

Bible Quotation: Paraphrase

Status: Approved

Scripts are basic guidelines for translation and recording into other languages. They should be adapted as necessary to make them understandable and relevant for each different culture and language. Some terms and concepts used may need more explanation or even be replaced or omitted completely.

Script Text

Siku ile Yesu alipofufuka, wanafunzi wake wawili walikuwa wanaenda mji jirani. Wakiendelea kutembea, walizungumza habari zilizotokea kumuhusu Yesu. Walitumaini kuwa alikuwa Masihi, lakini aliuawa. Wanawake waliwaambia yu hai anaishi tena. Nao hawakujua cha kuamini.

Yesu aliwakaribia na akaanza kutembea nao, lakini hawakumtambua. Aliwauliza juu ya mazungumzo yao, nao wakamueleza maajabu yote yaliyo tokea kumuhusu Yesu kwa siku chache zilizopita. Kwani walidhani wanaongea na mgeni asiyejua habari zilizotokea katika Yerusalemu.

Ndipo Yesu akawaelezea jinsi neno la Mungu linavyo sema kumuhusu Masihi. Aliwakumbusha manabii walivyosema, kwamba Masihi atateswa na kuuawa, na atafufuka tena siku ya tatu. Nao walipofika katika mji waliokuwa wamepanga kufikia hawa wanaume wawili, ilikuwa imekaribia jioni.

Hawa wanaume wawili walimkaribisha Yesu akae nao, naye akafanya hivyo. Walipokuwa tayari kula chakula cha jioni, Yesu alichukua kipande cha mkate, alimshukuru Mungu kwa mkate huo, akaumega. Ghafla, wakamtambua kuwa ni Yesu. Lakini wakati huo huo, Yesu akatoweka eneo hilo.

Hawa wanaume wawili waka ambiana, "Yule alikuwa ni Yesu! Ndiyo maana mioyo yetu ilikuwa inaungua wakati akielezea neno la Mungu kwetu." Punde, walirudi Yerusalemu. Nao walipofika, waliwaambia wanafunzi, "Yesu yu hai! tumemuona."

Wakati wanafunzi wanaendelea kuongea, Yesu alijitokeza katikati yao kwenye kile chumba na kusema, "Amani iwe kwenu!" Wanafunzi walidhani kuwa ni mzimu, lakini Yesu akawaambia, "Mbona mnaogopa na kuwa na mashaka? Angalieni mikono yangu na miguu. Mizimu haina mwili kama mimi." Kuwahakikishia kuwa Yeye si mzimu, aliwaomba chakula. Walimpa kipande cha samaki kilichopikwa, naye akala.

Yesu alisema, "Niliwaambia kila kitu kilicho andikwa katika neno la Mungu kunihusu mimi ni lazima kitimie." Ndipo alipofungua akili zao ili waweze kulielewa neno la Mungu. Akasema, "Iliandikwa muda mrefu uliopita yakuwa Masihi atateswa, atakufa na kufufuka kwa wafu siku ya tatu."

Iliandikwa pia katika maandiko kwamba wanafunzi, wangu watatangaza kwa kila mtu katika makundi, kwamba lazima watubu ili wapate msamaha wa dhambi zao. Nao watafanya hivyo kuanzia Yerusalem, nao wataenda kwa watu wote mahali pote. Ninyi ni mashahidi wa mambo haya.

Ndani ya siku arobaini zilizofuata, Yesu aliwatokea wanafunzi wake mara kwa mara. Wakati mwingine aliwatokea watu zaidi ya 500 kwa wakati mmoja! aliwadhibitishia wanafunzi wake kwa njia nyingi kuwa Yeye yu hai, na aliwafundisha kuhusu ufalme wa Mungu.

Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani. Kwa hiyo nendeni mkawafanye watu wote kuwa wanafunzi wangu, mkiwabatiza kwa jina la Mungu Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu, mkiwafundisha kuyatii yote niliyowaamuru. Kumbukeni kuwa nitakuwa pamoja nanyi siku zote."

Siku arobaini baada ya Yesu kufufuka kwa wafu, aliwaambia wanafunzi wake, "Kaeni Yerusalemu mpaka hapo Baba yangu atakapo wapa nguvu, pale Roho Mtakatifu atakapowajilia ninyi. Kisha Yesu akaenda mbinguni, nayo mawingu yakamfunika akatoweka kwao. Yesu alikaa mkono wa kuume wa Mungu kutawala vitu vyote.

Related information

Words of Life - Audio gospel messages in thousands of languages containing Bible based messages about salvation and Christian living.

Free downloads - Here you can find all the main GRN message scripts in several languages, plus pictures and other related materials, available for download.

The GRN Audio Library - Evangelistic and basic Bible teaching material appropriate to the people's need and culture in a variety of styles and formats.

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the right audio or video format - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?