unfoldingWord 28 - Kijana Tajiri Kiongozi

unfoldingWord 28 - Kijana Tajiri Kiongozi

Outline: Matthew 19:16-30; Mark 10:17-31; Luke 18:18-30

Script Number: 1228

Language: Swahili

Audience: General

Genre: Bible Stories & Teac

Purpose: Evangelism; Teaching

Bible Quotation: Paraphrase

Status: Approved

Scripts are basic guidelines for translation and recording into other languages. They should be adapted as necessary to make them understandable and relevant for each different culture and language. Some terms and concepts used may need more explanation or even be replaced or omitted completely.

Script Text

Siku moja, kiongozi kijana tajiri alimwendea Yesu na kumuuliza, "mwalimu mwema nifanye kitu gani cha lazima ili niwe na uzima wa milele?" Yesu akamwambia, "kwanini unaniita mwema?" Kuna mmoja tu aliye mwema naye ni Mungu. Lakini ukitaka kuwa na uzima wa milele, tii sheria za Mungu.

"Ni mambo gani nahitaji kutii?" Aliuliza. Yesu akajibu, "usiuwe. Usizini. Usiibe. Usidanganye. Mheshimu baba yako na mama yako, na umpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.

Lakini kijana akasema, "Nimezitii sheria hizo zote tangu nikiwa kijana. Je, nahitaji kufanya nini bado ili niishi milele? Yesu alimwangalia na akampenda.

Yesu akajibu, kama unataka kuwa mkamilifu, nenda ukauze kila kitu ulichonacho na utoe pesa kwa maskini, na utakuwa na hazina mbinguni, kisha njoo unifuate.

Yule kijana aliposikia alichokisema Yesu, alihuzunika sana, kwa sababu alikuwa tajiri sana na hakutaka kutoa vitu vyote alivyomiliki. Akageuka na akaenda mbali na Yesu.

Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Ni vigumu sana kwa watu matajiri kuingia katika ufalme wa Mungu! Ndiyo, ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano kuliko mtu tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu

Wanafunzi waliposikia alichosema Yesu, walishikwa na mshangao na kusema, "Ni nani basi anaweza kuokolewa?"

Yesu akawatazama wanafunzi na kusema, "Kwa watu mambo haya hayawezekani, lakini kwa Mungu mambo yote yanawezekana".

Petro akamwambia Yesu, "Tumeacha kila kitu na kukufuata wewe. Je, tutapata thawabu gani?"

Yesu akajibu, "Kila mmoja aliyeacha nyumba, kaka, dada yake, baba, mama, watoto, au mali kwa ajili yangu atapokea mara 100 zaidi na pia atapokea uzima wa milele. Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na wengi walio wa mwisho watakuwa wa kwanza."

Related information

Words of Life - Audio gospel messages in thousands of languages containing Bible based messages about salvation and Christian living.

Free downloads - Here you can find all the main GRN message scripts in several languages, plus pictures and other related materials, available for download.

The GRN Audio Library - Evangelistic and basic Bible teaching material appropriate to the people's need and culture in a variety of styles and formats.

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the right audio or video format - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?