unfoldingWord 45 - Stephano na Filipo

unfoldingWord 45 - Stephano na Filipo

Outline: Acts 6-8

Script Number: 1245

Language: Swahili

Audience: General

Genre: Bible Stories & Teac

Purpose: Evangelism; Teaching

Bible Quotation: Paraphrase

Status: Approved

Scripts are basic guidelines for translation and recording into other languages. They should be adapted as necessary to make them understandable and relevant for each different culture and language. Some terms and concepts used may need more explanation or even be replaced or omitted completely.

Script Text

Mmoja wa viongozi wa Kanisa la kwanza aliyeitwa Stephano. Alikuwa na tabia nzuri, mwenye kujawa na Roho Mtakatifu na hekima. Stephano alifanya miujiza mingi na kutumia ushawishi mkubwa illi watu wapate kumwamini Yesu.

Siku moja wakati Stephano anafundisha habari za Yesu, baadhi ya Wayahudi wasiomwamini Yesu walianza kubishana na Stephano. Walikasirika sana na kusema uongo kinyume cha Stephano kwa viongozi wa kidini. Wakasema, "Tumemsikia akisema vibaya juu ya Musa na Mungu!" Hivyo viongozi wa kidini walimkamata Stephano na kumpeleka kwa Kuhani Mkuu na viongozi wengine wa kiyahudi mahali ambapo mashahidi wengine zaidi walishuhudia uongo juu ya Stephano.

Kuhani Mkuu akamwuliza Stephano, "Maneno hayo ni ya kweli?" Stephano aliwajibu kwa kuwakumbusha mambo mengi makuu ambayo Mungu ameyafanya kutoka Ibrahimu hata wakati wa Yesu, jinsi ambavyo watu wa Mungu waliendelea kutomtii Mungu. Ndipo aliposema, "Enyi watu wagumu na waasi kila mara mnamkataa Roho Mtakatifu, kama wazazi wenu walivyomkataa Mungu na kuwaua manabii wake. Na nyinyi mmefanya jambo baya zaidi kuliko wao! Mmemwua Masihi."

Viongozi wa kidini ya kiyahudi waliposikia hayo, walikasirika, wakaziba masikio yao na kupaza sauti kubwa. Walimburuta Stephano kwa nguvu na kumpeleka nje ya mji na kumponda kwa mawe ili kumwua.

Stephano alipokaribia kufa, alilia kwa sauti, "Ee Yesu, pokea roho yangu." Ndipo alipopiga magoti na kusema tena, "Bwana, usiwahesabie dhambi hii." Baadaye akafa.

Kijana mmoja aitwaye Sauli alikubaliana na watu waliomwua Stephano na akalinda nguo zao walipokuwa wanamponda mawe. Tangu siku hiyo, watu wa Yerusalemu wakaanza kuwatesa wafuasi wa Yesu, hivyo waamini wakakimbia kwenda sehemu zingine. Licha ya hayo, walihubiri habari za Yesu popote walipoenda.

Mwanafunzi wa Yesu jina lake Filipo, alikuwa mmoja wa waumini waliokimbia kutoka Yerusalemu wakati wa mateso. Alienda Samaria alipohubiri habari za Yesu na watu wengi wakaokolewa. Ndipo siku moja malaika kutoka kwa Bwana akamwambia Filipo kwenda katika njia fulani jangwani. Alipokuwa akitembea barabarani, Filipo alimuona afisa mashuhuri kutoka nchi ya Ethiopia akiwa amepanda gari lake. Roho Mtakatifi alimwambia aende kukutana na kuzungumza na mtu huyo.

Filipo alipolikaribia gari, alimsikia mu-Ethiopia akisoma kile ambacho nabii Isaya aliandika. Huyo mtu alisoma, "Walimwongoza kama mwanakondoo na kumwua, kama mwanakondoo, alikaa kimya bila kusema neno. Walimtendea vibaya na hata hawakumheshimu. Walitoa uhai wake na kumwua."

Filipo alimwuliza huyo mtu wa Ethiopia, "Unaelewa kile unachokisoma?" Yule mtu akajibu, "Hapana. Siwezi kuelewa isipokuwa awepo mtu wa kunielezea. Tafadhali njoo ukae pamoja nami. Isaya aliandika kuhusu yeye au juu ya mtu mwingine?"

Filipo alimuelezea Muethiopia kuwa Isaya aliiandika juu ya Yesu. Vile vile Filipo alitumia maandiko mengine kumuelezea habari njema za Yesu.

Filipo na yule mtu wa Ethiopia walipokuwa wanasafiri, walifika kwenye maji. Muethiopia akasema, "Tazama! Kuna maji hapa! Je naweza kubatizwa?" Akamwambia dereva wake kusimamisha gari.

Kwa hiyo walienda kwenye maji, na Filipo akambatiza yule mtu wa Etheopia. Baada ya kutoka majini, ghafla Roho Mtakatifu alimwondoa Filipo na kumpeleka mahali pengine kuendelea kuwaambia watu habari za Yesu.

Yule mtu wa Ethiopia aliendelea na safari yake kwenda nyumbani akimfurahia za Mungu kuwa amemjua Kristo.

Related information

Words of Life - Audio gospel messages in thousands of languages containing Bible based messages about salvation and Christian living.

Free downloads - Here you can find all the main GRN message scripts in several languages, plus pictures and other related materials, available for download.

The GRN Audio Library - Evangelistic and basic Bible teaching material appropriate to the people's need and culture in a variety of styles and formats.

Choosing the audio or video format to download - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons