unfoldingWord 24 - Yohana Anambatiza Yesu

unfoldingWord 24 - Yohana Anambatiza Yesu

Esboço: Matthew 3; Mark 1; Luke 3; John 1:15-37

Número do roteiro: 1224

Idioma: Swahili

Público alvo: General

Tipo: Bible Stories & Teac

Propósito: Evangelism; Teaching

Passagem bíblica: Paraphrase

Estado: Approved

Os roteiros são guias básicos para a tradução e gravação em outros idiomas. Devem ser adaptados de acordo com a cultura e a língua de cada região, para fazê-lo relevante. Certos termos e conceitos podem precisar de uma explicação adicional ou mesmo serem omitidos no contexto de certos grupos culturais.

Texto do roteiro

Yohana mwana wa Zakaria na Elizabeth alikuwa na akawa nabii .Aliishi nyikani akila asali ya porini, nzige ,na kuvaa nguo zilizotengenezwa na manyoya ya ngamia.

Watu wengi walimfuata Yohana nyikani kumsikiliza.Aliwahubiri akisema,"tubuni kwa maana ufalme wa Mungu umekaribia"

Wakati watu waliposikia ujumbe wa Yohana wengi walitubu dhambi zao na kubatizwa .Viongozi wengi wa dini walikuja kubatizwa na Yohana lakini hawakutubu wala kuungama dhambi zao .

Yohana akawaambia viongozi wa dini" enyi nyoka wenye sumu! tubuni na kubadilisha tabia zenu.Kila mti usiozaa matunda mema hukatwa na kutupwa motoni. Yohana alitimiza kile kilichosemwa na manabii "angalia namtuma mjumbe wangu mbele yenu ambaye atawandalia njia zenu."

Baadhi ya Wayahudi wakamwuuliza Yohana kama yeye ni Kristo ,Yohana akajibu mimi siyo Kristo lakini kuna mmoja ajaye baada yangu ambaye ni mkuu sanakwani sistahili kufungua kamba ya viatu vyake .

Siku iliyofuata Yesu alikuja ili abatizwe na Yohana .Wakati alipomwona Yohana alisema,'angalia huyu ni mwanakondoo wa Mungu atakayechukua dhambi ya ulimwengu.

Yohana akamwambia Yesu mimi sistahili kukubatiza wewe ila wewe unastahili kunibatiza mimi.Lakini Yesu akasema "ni lazima kunibatiza mimi kwa sababu ni kitu sahihi kwa hiyo Yohana akambatizaYesu pamoja na kwamba Yesu hakuwahi kutenda dhambi.

Wakati Yesu alipotoka majini baada ya kubatizwa Roho wa Mungu alitokea katika umbo la njiwa alishuka akatulia juu yake.Wakati huo sauti ya Mungu ikaongea kutoka mbinguni na kusema "Wewe ni mwanangu ambaye ninakupenda na ninayependezwa naye ".

Mungu akamwambia Yohana," Roho wa Mungu atakuja juu ya mtu ambaye umembatiza .Na mtu huyo ni mwana wa Mungu ,"Kuna Mungu mmoja tu.Lakini wakati Yohana alipokuwa akimbatiza Yesu alisikia Baba Mungu akisema na akamuona Mungu mwana ,ambaye ni Yesu ,na akamwona Roho Mtakatifu.

Informações pertinentes

Palavras de Vida - A GRN tem mensagens evangelísticas em áudio em milhares de idiomas contendo a mensagem bíblica sobre a salvação e a vida cristã.

Downloads gratuitos - Baixe gratuitamente áudios de histórias bíblicas e estudos em milhares de idiomas, além de ilustrações, roteiros e vários outros tipos de material para evangelismo e crescimento da igreja.

Coleção de áudio da GRN - Material evangelístico e de ensino bíblico, adaptado às necessidades e cultura de cada povo em vários estilos e formatos.

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the right audio or video format - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?