unfoldingWord 44 - Petro na Yohana Wamponya Ombaomba

unfoldingWord 44 - Petro na Yohana Wamponya Ombaomba

Esquema: Acts 3-4:22

Número de guión: 1244

Idioma: Swahili

Audiencia: General

Tipo: Bible Stories & Teac

Propósito: Evangelism; Teaching

Citación Biblica: Paraphrase

Estado: Approved

Los guiones son pautas básicas para la traducción y grabación a otros idiomas. Deben adaptarse según sea necesario para que sean comprendidas y relevantes para cada cultura e idioma diferentes. Algunos términos y conceptos utilizados pueden necesitar más explicación o incluso ser reemplazados o omitidos por completo.

Guión de texto

Siku moja, Petro na Yohana walikuwa wakihudhuria Hekaluni. Na walipokaribia kwenye lango la hekalu, walimwona kiwete aliyeketi langoni na kuomba fedha.

Petro akamtazama yule kiwete na kumwambia, "Sina fedha za kukupa. Japo nitakupa kile nilichonacho. Kwa jina la Yesu Kristo, simama na utembee!"

Mara tu, Mungu akamponya yule kiwete akaamka na akaanza kutembea na kurukaruka hapa na pale na kumsifu Mungu. Watu wote waliokuwa kwenye ua wa Hekalu walishikwa na mshangao mkubwa.

Watu wengi wakakusanyika kwa haraka ili kumwona yule kiwete aliyeponywa. Petro akawaambia, "Kwa nini mnashangazwa na uponyaji ambao mtu huyu ameupata? Uponyaji huu haujafanyika kwa sababu ya wema na nguvu zetu. Bali ni kwa nguvu na imani itokayo kwa Yesu Kristo."

Ninyi ndio mliomshawishi Mtawala kutoka Rumi kumuua Yesu. Mlimuua mwanzilishi wa uzima, lakini Mungu alimfufua katika wafu. Ingawa hamkujua kile mlichokuwa mkikifanya, Mungu alitumia matendo yenu maovu kwa kutimiza unabii wa kwamba Masihi atateswa na kufa. Kwa hiyo mnapaswa kutubuna kurudi kwa Mungu ili msamehewe dhambi zenu.

Viongozi wengi wa Hekalu walisikitishwa sana na yale maneno ya Petro na Yohana. Kwa hiyo wakawakamata na kuwaweka gerezani. Pamoja na hayo, bado watu wengi walimwamini Yesu kwa ujumbe wa Petro, na idadi ya wanaume waliomwamini Yesu siku hiyo walikuwa 5,000.

Siku iliyofuata, viongozi wa hekalu waliwaleta Petro na Yohana kwa kuhani mkuu na mbele ya viongozi wa kidini na kuwauliza, "Ni kwa nguzu gani mlimponya huyu kiwete?"

Petro akawajibu, " Mtu huyu asimamaye mbele yenu, aliponywa kwa nguzu za Yesu. Ambaye nyinyi mlimsulubisha, lakini Mungu alimfufua katika wafu. Hamkumkubali, ila hakuna njia jingine duniani inayoweza kuokoa isipokuwa kwa nguvu za Yesu Kristo!"

Wale viongozi wa dini walipowatazama na kuwasikiliza Petro na Yohana na ujasiri wa hotuba yao, na kuowaona kuwa walikuwa watu wa kawaida na wasio na elimu, walishitushwa. Walikumbuka kuwa walikuwa pamoja na Yesu Kristo. Baada ya kuwatisha waliwaruhusu waende zao.

Información relacionada

Palabras de Vida - GRN tiene mensajes audios en miles de idiomas que contienen mensajes basados en la Biblia acerca de la salvación y la vida cristiana.

Descargas gratis - Aquí puede encontrar los guiones principales de GRN en varios idiomas y también imágenes y otros materiales relacionados. Todos están disponibles para descargar.

Librería de audio de GRN - Material evangelistico y de enseñanza adecuado a las necesidades y a la cultura en variedad de stilos y formatos

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the right audio or video format - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?