unfoldingWord 43 - Kanisa Linaanza

unfoldingWord 43 - Kanisa Linaanza

Esquema: Acts 1:12-14; 2

Número de guión: 1243

Idioma: Swahili

Audiencia: General

Tipo: Bible Stories & Teac

Propósito: Evangelism; Teaching

Citación Biblica: Paraphrase

Estado: Approved

Los guiones son pautas básicas para la traducción y grabación a otros idiomas. Deben adaptarse según sea necesario para que sean comprendidas y relevantes para cada cultura e idioma diferentes. Algunos términos y conceptos utilizados pueden necesitar más explicación o incluso ser reemplazados o omitidos por completo.

Guión de texto

Baada ya Yesu kurudi mbinguni, wanafunzi wake walibaki Yerusalem kama alivyowaagiza kufanya. Waumini wake walikuwa na utaratibu wa kukusanyika na kuomba pamoja.

Kila mwaka baada ya siku 50 za Pasaka, Wayahudi walisheherekea siku muhimu ya Pentekosti. Pentekosti ni kipindi ambacho wayahudi walisheherekea mavuno ya ngano, Wayahudi walikwenda Yerusalemu wakitokea ulimwenguni kote kusheherekea kwa pamoja Pentekosti. Mwaka huu kipindi cha Pentekosti kilikuwa baada ya wiki moja Yesu aliporudi mbinguni.

Wakati waumini wakiwa pamoja, ghafla nyumba ilijawa na sauti kama upepo mkali. Kisha kitu kama mwali wa moto kikaonekana juu ya vichwa vya waumini wote. Wote walijazwa na Roho Mtakatifu na kuanza kunena kwa lugha nyingine.

Watu wa Yerusalemu waliposikia kelele, kusanyiko la watu walikuja kushuhudia kilichotokea. Watu waliposikia waumini wakitangaza matendo ya ajabu ya kazi za Mungu, walishangaa sana kwa kuwa walisikia maneno hayo kwa lugha zao za asili.

Baadhi ya watu wakawashutumu wanafunzi kuwa wamelewa, lakini Petro akasimama akawaambia, nisikilizeni, hawa watu hawajalewa, bali unatimizwa unabii uliotolewa na Yoeli ambao Mungu alisema "Siku za mwisho nitamdhihirisha Roho"

Wanaume wa Israeli Yesu alikuwa mwanadamu alitenda miujiza na maajabu mengi kwa uwezo wa Mungu, nanyi mnajua na kuona lakini mlimsulubisha.

Ingawa Yesu alikufa, Mungu alimfufua kutoka kwa wafu na hii inatimiza unabii unaosema "Hutamwacha mtakatifu wako kuoza kaburini" Nasi tu mashahidi wa mambo hayo kuwa ukweli kwamba Mungu alimfufua Yesu.

Yesu anatukuzwa kwenye mkono wa kuume wa Mungu baba, na Yesu amemtuma Roho Mtakatiifu kama alivyoahidi kuwa angefanya. Roho Mtakatifu anasababisha mambo mnayoyaona na kuyasikia.

"Mlimsulubisha mtu huyu Yesu. Lakini mfahamu kwa uhakika Mungu amesababisha Yesukufanyika kuwa Bwana na Masihi.

Watu waliomsikiliza Petro walivutwa kwa undani na mafundisho aliyosema. Wakamwuliza Petro na wanafunzi. Je mnataka tufanye nini?

Petro akawajibu, "kila mtu anapaswa atubu na kubatizwa kwa Jina la Yesu Kristo na Mungu atawasamehe dhambi zenu. Kisha atawapa kipawa cha Roho Mtakatifu."

Yapata Watu 3,000 wakaamini alichokisema Petro wakawa wanafunzi wa Yesu. Nao wakabatizwa wakawa washirika wa kanisa la Yerusalemu.

Wanafunzi waliendelea kusikiliza mafundisho ya mitume, walikaa pamoja na kula pamoja na kuomba pamoja. Walifurahi wakamsifu Mungu kwa pamoja na walishirikishana kila kitu walichokuwa nacho kwa pamoja. Kila mtu alikuwa na mtizamo mzuri juu yao. kila siku watu wengi waliendelea kuamini.

Información relacionada

Palabras de Vida - GRN tiene mensajes audios en miles de idiomas que contienen mensajes basados en la Biblia acerca de la salvación y la vida cristiana.

Descargas gratis - Aquí puede encontrar los guiones principales de GRN en varios idiomas y también imágenes y otros materiales relacionados. Todos están disponibles para descargar.

Librería de audio de GRN - Material evangelistico y de enseñanza adecuado a las necesidades y a la cultura en variedad de stilos y formatos

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the right audio or video format - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?