unfoldingWord 37 - Yesu Amfufua Lazaro kutoka Wafu

unfoldingWord 37 - Yesu Amfufua Lazaro kutoka Wafu

Esquema: John 11:1-46

Número de guión: 1237

Idioma: Swahili

Audiencia: General

Tipo: Bible Stories & Teac

Propósito: Evangelism; Teaching

Citación Biblica: Paraphrase

Estado: Approved

Los guiones son pautas básicas para la traducción y grabación a otros idiomas. Deben adaptarse según sea necesario para que sean comprendidas y relevantes para cada cultura e idioma diferentes. Algunos términos y conceptos utilizados pueden necesitar más explicación o incluso ser reemplazados o omitidos por completo.

Guión de texto

Siku moja, Yesu alipata habari kuwa Lazaro ni mgonjwa sana. Lazaro na dada zake wawili- Martha na Maria walikuwa marafiki wa karibu wa Yesu. Yesu alipopata habari hizi alisema, "Huu si ugonjwa wa kifo, bali ni ugonjwa wa kumtukuza Mungu." Yesu aliwapenda marafiki zake, lakini alisubiri hadi siku mbili.

Baada ya siku mbili, Yesu aliwaambia wanafunzi wake, ''Twendeni tena Uyahudi." "Lakini mwalimu. " Wanafunzi wake walisema, "Muda mfupi tu uliopita watu walitaka kukuua!" Yesu alisema "Rafiki yetu Lazaro amelala usingizi na ni lazima nimwamshe."

Wanafunzi wa Yesu walijibu, "Bwana, kama Lazaro amelala, basi atapata nafuu." Yesu aliwaambia wazi, "Lazaro amekufa, nafurahi kuwa sikuwepo ili mpate kuniamini."

Yesu alipofika katika mji wa Lazaro, Lazaro alikuwa tayari amekufa kwa siku nne. Martha alikwenda kumwona Yesu akasema, "Bwana, kama ungekuwa hapa, kaka yangu asingekufa . Lakini ninaamini kuwa Mungu atakupa chochote umwombacho."

Yesu akajibu akasema, "Mimi ni Ufufuo na Uzima, yeyote aniaminiye ataishi, hata kama akifa. Kila aniaminiye hatakufa. Unaamini hivyo?" Martha akajibu, "Ndiyo Bwana ninaamini kuwa wewe ni Masihi, Mwanawa Mungu."

Maria alipofika. Alianguka miguuni pa Yesu akasema, "Bwana, kama wewe tu ungekuwepo kaka yangu asingekufa." Yesu akawauliza, "Mmemuweka wapi Lazaro?" Walimjibu " Kaburini, njoo uone." Yesu alilia.

Kaburi lilikuwa pango limefunikwa na jiwe. Yesu alipofika kaburini aliwaambia, "Liondoeni jiwe." Lakini Martha alisema, "Amekuwa kaburini sasa siku nne, ananuka!"

Yesu alijibu, "Je, sikusema kuwa kama ukiniamini utaona utukufu wa Mungu?" Ndipo wakaliondoa jiwe.

Basi Yesu alitazama juu mbinguni akasema, "Baba, asante kwa kuwa unanisikia. Tena najua wewe hunisikia siku zote. Lakini nimesema haya kwa ajili ya watu hawa waliosimama hapa, kwa kuwa wataamini kuwa ulinituma." Kisha Yesu akapaza sauti, "Lazaro, njoo nje."

Ndipo Lazaro alitoka nje! Alikuwa bado amefungwa sanda, Yesu akawaambia, "Msaidieni kuondoa sanda na mwacheni huru!." Wayahudi wengi walimwamini Yesu kwa sababu ya muujiza huu.

Lakini viongozi wa dini ya kiyahudi waliona wivu, ndipo wakakusanyika pamoja kupanga watakavyoweza kumuua Yesu na Lazaro.

Información relacionada

Palabras de Vida - GRN tiene mensajes audios en miles de idiomas que contienen mensajes basados en la Biblia acerca de la salvación y la vida cristiana.

Descargas gratis - Aquí puede encontrar los guiones principales de GRN en varios idiomas y también imágenes y otros materiales relacionados. Todos están disponibles para descargar.

Librería de audio de GRN - Material evangelistico y de enseñanza adecuado a las necesidades y a la cultura en variedad de stilos y formatos

Choosing the audio or video format to download - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons