unfoldingWord 27 - Simulizi ya Msamaria Mwema

unfoldingWord 27 - Simulizi ya Msamaria Mwema

Esquema: Luke 10:25-37

Número de guión: 1227

Idioma: Swahili

Audiencia: General

Tipo: Bible Stories & Teac

Propósito: Evangelism; Teaching

Citación Biblica: Paraphrase

Estado: Approved

Los guiones son pautas básicas para la traducción y grabación a otros idiomas. Deben adaptarse según sea necesario para que sean comprendidas y relevantes para cada cultura e idioma diferentes. Algunos términos y conceptos utilizados pueden necesitar más explicación o incluso ser reemplazados o omitidos por completo.

Guión de texto

Siku moja Mwalimu wa mambo ya sheria ya Kiyahudi alimwendea Yesu na kumuuliza kwa kumjaribu akisema,"Mwalimu nifanyeje ili ni urithi uzima wa milele?" Yesu akamjibu " sheria ya Mungu imeandikwaje?"

Mwalimu wa mambo ya sheria ya Kiyahudi alimjibu Yesu na kusema, sheria ya Mungu inasema "Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa nafsi yako yote, kwa nguvu zako zote na kwa akili zako zote. Na pia inasema "Mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe. Yesu akamwambia "uko sahihi. Fanya hivyo na utaurithi uzima wa milele."

Lakini huyu Mwalimu wa mambo ya sheria ya Kiyahudi akitaka kujionyesha kwamba yeye ni mwenye haki, alimuuliza Yesu; "Jirani yangu ni nani?"

Yesu alimjibu huyu Mwalimu wa mambo ya sheria ya Kiyahudi kwa kumpa simulizi. " Kulikuwa na Myahudi mmoja aliyekuwa anasafiri kwa barabara kutoka Yerusalemu kwenda Yeriko.

Wakati Myahudi huyu alipokuwa akisafiri kikundi cha wezi kilimvamia na kumwibia kila kitu na kumpiga sana karibu ya kufa. Walipokuwa wamempiga sana karibu ya kufa, walimwacha hapo barabarani na kuondoka zao.

Muda mfupi baada ya tukio hilo Kuhani wa Kiyahudi alikuwa akisafiri na kupitia katika barabara hii ambayo Myahudi yule alikuwa amepigwa na kuachwa pale. Alipomuona alipita upande mwingine wa barabara mbali na alipokuwepo mtu huyo na kuendelea na safari yake wala asimjali na kumsaidia mtu yule.

Baada ya muda mfupi Mlawi (Walawi walikuwa kabila la Wayahudi ambao lilikuwa linawasadia makuhani katika huduma hekaluni) naye alipita barabara hiyohiyo na alipomuona mtu yule aliyekuwa amepigwa na kuumizwa na wezi alipita upande mwingine wa barabara na kuendelea na safari yake bila kumjali.

Mtu mwingine aliyepita barabara hiyo alikuwa ni Msamaria (Wasamaria walikuwa wa uzao wa Wayahudi na ni watu waliooa na kuolewa na watu wa mataifa mengine. Wasamaria walikuwa wanachukiana sana na Wayahudi). Huyo Msamaria alipomuona Myahudi yule aliyekuwa amepigwa na kuumizwa sana na wezi, alimuonea sana huruma. Alimchukua na kuyahudumia majeraha yake na kumfunga pandeji.

Msamaria baada ya hapo alimchukua huyo Myahudi na kumpandisha kwenye Punda wake na kumpeleka kwenye nyumba ya wageni iliyokuwa karibu na barabara na kumuhudumia zaidi.

Siku iliyofuata Msamaria huyu alihitaji kuendelea na safari yake na hivyo alimkabidhi yule muangalizi wa nyumba ya wageni na kumwambia " Mhudumie Myahudi huyu aliyepigwa na wezi. Akampa fedha yule muangalizi na kumwambia, kama utatumia fedha zaidi katika kumhudumia Myahudi huyu basi nikirudi kutoka safari yangu nitakuja nilipe kiasi kilichoongezeka.

Baada ya hadithi hiyo, Yesu alimuuliza yule Mwalimu wa mambo ya sheria ya Kiyahudi, kwamba "Unafikiri katika watu hao watatu, ni nani aliyekuwa jirani yake yule Myahudi aliyepigwa na wezi?" Yule Mwalimu wa mambo ya sheria ya Kiyahudi alijibu na kumwambia Yesu "ni yule aliyemuonea huruma". Yesu akamwambia "Wewe nawe nenda kafanye vivyo hivyo."

Información relacionada

Palabras de Vida - GRN tiene mensajes audios en miles de idiomas que contienen mensajes basados en la Biblia acerca de la salvación y la vida cristiana.

Descargas gratis - Aquí puede encontrar los guiones principales de GRN en varios idiomas y también imágenes y otros materiales relacionados. Todos están disponibles para descargar.

Librería de audio de GRN - Material evangelistico y de enseñanza adecuado a las necesidades y a la cultura en variedad de stilos y formatos

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the right audio or video format - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?