unfoldingWord 05 - Mtoto wa Ahadi

unfoldingWord 05 - Mtoto wa Ahadi

Esquema: Genesis 16-22

Número de guión: 1205

Idioma: Swahili

Audiencia: General

Tipo: Bible Stories & Teac

Propósito: Evangelism; Teaching

Citación Biblica: Paraphrase

Estado: Approved

Los guiones son pautas básicas para la traducción y grabación a otros idiomas. Deben adaptarse según sea necesario para que sean comprendidas y relevantes para cada cultura e idioma diferentes. Algunos términos y conceptos utilizados pueden necesitar más explicación o incluso ser reemplazados o omitidos por completo.

Guión de texto

Baada ya kuishi miaka kumi katika nchi ya Kaanani, Abraham na Sarai hawakuwa na mtoto. Sarai mke wa Abraham akamwambia," kwa kuwa Mungu hajanipa mtoto nami ni mzee sana siwezi kupata mtoto. Mchukue Hajiri mjakazi wangu umwoe ili anizalie mtoto."

Hivyo Abraham akamwoa Hajiri. Hajiri akapata mtoto wa kiume, Abrahamu akampa jina Ishmaeli. Lakini Sarai akamwonea wivu Hajiri. Alipotimiza umri wa miaka kumi na tatu, Mungu akaongea na Abrahamu.

Mungu akasema, "Mimi ni Mungu mkuu. nitafanya agano pamoja nawe. "Kisha Abrahamu akasujudu. Pia Mungu akamwambia Abrahamu, "Utakuwa baba wa mataifa mengi. Nitakupatia wewe na uzao wako nchi ya kanaani kuwa miliki yao na nitakuwa Mungu wao milele. Nawe utawatairi wanaume wote wa familia yako."

Mkeo Sarai, atapata mtoto wa kiume, atakuwa mtoto wa ahadi. Utamwita Isaka. Nitafanya Agano langu pamoja naye. Naye atakuwa taifa kubwa. Nitamfanya Ishmaeli kuwa Taifa kubwa pia. Lakini Agano langu litakuwa pamoja na Isaka. "Kisha Mungu akabadili jina la Abrahamu kuwa Ibrahimu, maana ya jina hilo ni "baba wa wengi." Mungu pia akabadili jina la Sarai kuwa Sara, maana yake "mtoto wa mfalme ."

Siku hiyo Abrahamu akawatairi wanaume wote wa nyumba yake. Baada ya mwaka mmoja, Ibrahimu alitimiza miaka 100 na Sara miaka 90, Sara akazaa na Ibrahimu mtoto wa kiume. Wakamwita jina lake Isaka kama Mungu alivyowaagiza.

Isaka alipokuwa kijana, Mungu akaijaribu imani ya Ibrahimu na kumwambia, "Mchukue, Isaka kijana wako wa pekee, na umuue kama sadaka ya kuteketezwa kwa ajili yangu. "Ibrahimu alimtii Mungu na kumwandaa kijana kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa.

Ibrahimu na Isaka walipokuwa wakitembea kuelekea eneo la kutoa sadaka, Isaka akauliza. "Baba, kuni kwa ajili ya sadaka tunazo, lakini kondoo yuko wapi?" Ibrahimu akajibu. "Mungu atajipatia kondoo kwa ajili ya sadaka, mtoto wangu."

Walipofika eneo la kutoa sadaka, Ibrahimu akamfunga kijana wake Isaka na kumlaza juu ya mazabahu. Alikuwa anajiandaa kumwua kijana wake Mungu akasema, "Acha! Usimdhuru kijana! Sasa natambua unaniogopa mimi kwa sababu hukumwacha kijana kwa ajili yangu."

Karibu naye, Ibrahimu akaona kondoo amejinasa kwenye kichaka. Mungu akampatia kondoo kuwa sadaka ya kuteketezwa badala ya Isaka. Ibrahimu kwa furaha akamtoa kondoo kuwa sadaka ya kutekezwa.

Kisha Mungu akamwambia Ibrahimu. "Kwa sababu ulikuwa tayari kutoa kila kitu kwa ajili yangu hata kijana wako wa pekee, naahidi kukubariki wewe. Uzao wako utaongezeka zaidi kama nyota za angani. Kwa sababu umenitii mimi, familia zote ulimwenguni watabarikiwa kwa sababu ya familia yako ."

Información relacionada

Palabras de Vida - GRN tiene mensajes audios en miles de idiomas que contienen mensajes basados en la Biblia acerca de la salvación y la vida cristiana.

Descargas gratis - Aquí puede encontrar los guiones principales de GRN en varios idiomas y también imágenes y otros materiales relacionados. Todos están disponibles para descargar.

Librería de audio de GRN - Material evangelistico y de enseñanza adecuado a las necesidades y a la cultura en variedad de stilos y formatos

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the right audio or video format - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?