unfoldingWord 01 - Uumbaji

unfoldingWord 01 - Uumbaji

Esquema: Genesis 1-2

Número de guión: 1201

Idioma: Swahili

Tema: Bible timeline (Creation)

Audiencia: General

Tipo: Bible Stories & Teac

Propósito: Evangelism; Teaching

Citación Biblica: Paraphrase

Estado: Approved

Los guiones son pautas básicas para la traducción y grabación a otros idiomas. Deben adaptarse según sea necesario para que sean comprendidas y relevantes para cada cultura e idioma diferentes. Algunos términos y conceptos utilizados pueden necesitar más explicación o incluso ser reemplazados o omitidos por completo.

Guión de texto

Hivi ndivyo mwanzo wa kila kitu ulivyotokea. Mungu aliumba ulimwengu na vitu vyote katika siku sita. Maana nchi ilikuwa giza na tupu, na hakuna kilichokuwa kimeumbwa. Lakini Roho ya Mungu ilikuwa juu ya maji.

Ndipo Mungu akasema, "Na iwe mwanga." Na ikawa hivyo, Mungu aliona kuwa mwanga ni mzuri na akauita mchana, na akatenganisha kutoka giza, akauita usiku. Mungu aliumba mwanga siku ya kwanza ya uumbaji.

Siku ya pili ya uumbaji, Mungu alisema na kuumba anga juu ya dunia. Aliumba anga kwa kutenganisha na maji ya juu kutoka maji ya chini.

Siku ya tatu, Mungu alisema na kutenganisha maji na nchi kavu. Nchi kavu akaiita "dunia," na maji akayaita "bahari." Mungu aliona kila kitu alichokiumba ya kuwa ni chema.

Ndipo Mungu akasema, "Nchi izae aina zote za miti na mimea." Na ndivyo ilivyotokea. Mungu aliona kila kitu alichokiumba ni chema.

Katika siku ya nne ya uumbaji, Mungu alisema na kuumba jua, mwezi na nyota. Mungu aliviumba ili kuleta mwanga duniani na kuonesha mchana na usiku, nyakati na miaka. Mungu aliona alichokiumba ni chema.

Siku ya tano, Mungu alisema na kuumba vitu vyote viishivyo majini na ndege wote. Mungu aliona kuwa ni vyema, na akavibariki.

Siku ya sita ya uumbaji, Mungu alisema, "Na iwe wanyama wa aina zote katika nchi." Na ilitokea kama Mungu alivyosema. Wengine walikuwa wa shambani, wengine wa kutambaa na wa porini. Na ilitokea kama yeye alivyotamka. Na Mungu aliona kwamba ilikuwa ni vyema.

Ndipo Mungu akasema, "Na tumfanye mtu kwa mfano wetu kuwa kama sisi. Watakuwa na mamlaka juu ya dunia na wanyama wote."

Mungu alichukua vumbi, akamfanya mtu, na akapulizia uhai ndani yake. Akamwita Adamu kwa jina lake. Akatengeneza bustani ya Edeni akamweka aishi humo, na aitunze.

Katikati ya bustani, Mungu alipanda miti miwili muhimu- mti wa uzima na wa ujuzi wa mema na mabaya. Mungu alimwambia Adamu anaweza kula aina zote za miti isipokuwa mti wa ujuzi wa mema na mabaya. Kama akila tunda la mti huu, atakufa.

Mungu alisema, "Si vyema mtu kuwa peke yake." Lakini hakuna hata mnyama mmoja aliyeweza kuwa msaidizi wa Adamu.

Ndipo Mungu alimletea Adamu usingizi mzito. Akatoa ubavu mmoja kwa Adamu na kutengeneza mwanamke na akamleta kwake.

Adamu alipomwona, alisema, "Angalau! Huyu ni kama mimi! Ataitwa 'mwanamke' maana ametoka kwa mwanaume." Kwa maana mwanaume atamwacha baba na mama yake watakuwa pamoja na mkewe.

Mungu aliumba mwanamke na mwanaume kwa mfano wake. Akawabariki akasema, "zaeni watoto na wajukuu mkaijaze dunia." Mungu aliona kila kitu alichokifanya ni chema sana, na alifurahishwa sana na kila kitu. Hii ilitokea katika siku ya sita ya uumbaji wake.

Siku ya saba ilipofika, Mungu alikuwa amemaliza kazi yake.Hivyo Mungu alipumzika katika kila alichokifanya. Aliibariki siku ya saba akaifanya takatifu kwa sababu katika siku hii alipumzika. Hivyo ndivyo Mungu alivyoumba ulimwengu na kila kitu ndani yake.

Información relacionada

Palabras de Vida - GRN tiene mensajes audios en miles de idiomas que contienen mensajes basados en la Biblia acerca de la salvación y la vida cristiana.

Descargas gratis - Aquí puede encontrar los guiones principales de GRN en varios idiomas y también imágenes y otros materiales relacionados. Todos están disponibles para descargar.

Librería de audio de GRN - Material evangelistico y de enseñanza adecuado a las necesidades y a la cultura en variedad de stilos y formatos

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the right audio or video format - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?