Dil seçin

mic

unfoldingWord 40 - Yesu Anasulubiwa

unfoldingWord 40 - Yesu Anasulubiwa

Kontur: Matthew 27:27-61; Mark 15:16-47; Luke 23:26-56; John 19:17-42

Skript nömrəsi: 1240

Dil: Swahili

Tamaşaçılar: General

Məqsəd: Evangelism; Teaching

سمات: Bible Stories; Paraphrase Scripture

Vəziyyət: Approved

Skriptlər digər dillərə tərcümə və qeyd üçün əsas təlimatlardır. Onlar hər bir fərqli mədəniyyət və dil üçün başa düşülən və uyğun olması üçün lazım olduqda uyğunlaşdırılmalıdır. İstifadə olunan bəzi terminlər və anlayışlar daha çox izahat tələb edə bilər və ya hətta dəyişdirilə və ya tamamilə buraxıla bilər.

Skript Mətni

Baada ya askari kumdhihaki Yesu, walimpeleka kumsulibisha. walimlazimisha aubebe msalaba ambao ungetumika kumuua.

Askari walimpeleka Yesu eneo liitwalo "fuvu la kichwa" wakaipigilia miguu na mikono yake msalabani. Lakini Yesu akasema, "Baba wasamehe, kwa sababu hawajui wanalotenda." Pilato akaagiza waandike kwamba, "Mfalme wa Wayahudi" ikiwa ni ishara; na waweke msalabani, juu ya kichwa cha Yesu.

Askari walipigia kura mavazi yake. Na kitendo hiki kinatimiza unabii usemao kwamba, " wakagawana nguo zangu na kucheza kamali."

Yesu alisulibiwa katikati ya wanyang'anyi wawili; mmojawapo alimdhihaki Yesu, lakini mwingine alisema, "Humwogopi Mungu!? Sisi tunahatia, lakini huyu hana hatia" Ndipo yeye akamwabia Yesu "Tafadhali unikumbuke katika ufalme wako" Yesu akamjibu, leo, utakuwa nami Paradiso."

Viongozi wa wayahudi na baadhi ya wengine katika umati walimdhihaki Yesu. Wakisema, "kama wewe ni Mwana wa Mungu, shuka msalabani, jiokoe mwenyewe, ndipo tutakuamini."

Ndipo katika eneo hilo kukawa giza nene, ingawa ilikuwa mchana. Mchana huo kukawa giza kwa saa tatu.

Yesu akalia, "Baba imekwisha naweka mikononi mwako roho yangu." Ndipo akainama akajitoa mwenyewe roho yake. Alipokufa lilitokea tetemeko la ardhi na pazia la hekaluni lililowatenga watu na Mungu lilipasuka vipande viwili, tokea juu hadi chini.

Kifo chake Yesu kinafungua njia ili watu waje kwa Mungu. Askari aliyemlinda Yesu alipoona mambo haya yote yanatokea alisema, "Hakika mtu huyu hakuwa na hatia, alikuwa Mwana wa Mungu."

Na ndipo Yusufu na Nikodemo viongozi wa Wayahudi walioamini Yesu kuwa ni Masihi wakauomba mwili wa Yesu na kuufunga kwenye sanda na kupeleka kwenye kaburi lililochongwa tayari mwambani na wakasogeza jiwe kubwa kulifunga kaburi.

Əlaqədar məlumat

Həyat Sözləri - Xilas və xristian həyatı haqqında Müqəddəs Kitaba əsaslanan mesajları ehtiva edən minlərlə dildə audio müjdə mesajları.

Choosing the audio or video format to download - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?

Copyright and Licensing - GRN shares its audio, video and written scripts under Creative Commons