unfoldingWord 34 - Yesu Anafundisha Mambo Mengine

unfoldingWord 34 - Yesu Anafundisha Mambo Mengine

Raamwerk: Matthew 13:31-46; Mark 4:26-34; Luke 13:18-21;18:9-14

Skripnommer: 1234

Taal: Swahili

Gehoor: General

Genre: Bible Stories & Teac

Doel: Evangelism; Teaching

Bybelaanhaling: Paraphrase

Status: Approved

Skrips is basiese riglyne vir vertaling en opname in ander tale. Hulle moet so nodig aangepas word dat hulle verstaanbaar en relevant is vir elke verskillende kultuur en taal. Sommige terme en konsepte wat gebruik word, het moontlik meer verduideliking nodig of selfs heeltemal vervang of weggelaat word.

Skripteks

Yesu aliwaambia masilimuzi mengi kuhusu ufalme wa Mungu .Kwa mfano,alisema,"Ufalme wa Mungu ni kama punje ya haradali ambayo mtu aliipanda shambani mwake.Unajua kwamba punje ya haradali ni ndogo kuliko punje zote."

Lakini wakati punje ya haradali inapokuwa, inakuwa kubwa kuliko mimea yote bustanini, inakuwa na ukubwa wa kutosha hata ndege huja na kutua kwenye matawi yake,

Yesu akawaambia simulizi nyingine ,"Ufalme wa Mungu ni kama amira aliyoichanganya mwanamke kwenye baadhi ya donge la mkate na mpaka kusambaa kwenye donge lote."

Ufalme wa Mungu pia unafanana kama hazina ambayo mtu ameificha shambani.Mtu mwingine akaikuta hazina hiyo na kuifukia tena. Alijawa na furaha kiasi kwamba akaenda kuuza kila kitu alichonacho na akatumia fedha hiyo kununua shamba hilo.

Ufalme wa Mungu pia ni kama lulu kamili ya thamani kubwa .Mfanyabiashara wa lulu alipoipata, aliuza vitu vyote alivyokuwanavyo na kutumia fedha hiyo kununua hiyo lulu.

Tena Yesu akawaambia simulizi ya baadhi ya watu ambao wameweka tumaini katika matendo yao mema na kudharau watu wengine .Akasema. "Watu wawili walikwenda hekaluni kusali .Mmoja alikuwa mtoza ushuru na mwingine kiongozi wa dini.

Kiongozi wa dini aliomba hivi. 'Asante, Mungu kwamba mimi siyo mwenye dhambi kama watu wengine - mfano wanyanganyi, wasio haki, wazinzi, au hata kama huyu mtoza ushuru'".

"Kwa mfano, nafunga mara mbili kwa wiki na kukutolea moja ya kumi ya pesa zote na mali zote nizipatazo.

Lakini mtoza ushuru alisimama mbali na kiongozi wa dini hata hakuelekeza uso wake mbinguni. Badala yake alijipiga ngumi kifua chake na akaomba, "Mungu, tafadhali unirehemu mimi kwa sababu ni mwenye dhambi.

Kisha Yesu akasema, "Lakini nawaambieni ukweli, Mungu alisikia maombi ya mtoza ushuru na kumtangaza kuwa mwenye haki. Lakini hakuyapenda maombi ya kiongozi wa dini. Mungu humshusha kila ajikwezae na humpandisha kila ajinyenyekezaye,

Verwante inligting

Woorde van Lewe - GRN het oudio-evangelieboodskappe in duisende tale wat Bybelgebaseerde boodskappe bevat oor verlossing en Christelike lewe.

Gratis aflaaie - Hier vind u al die belangrikste GRN boodskap skrips in verskeie tale, plus prente en ander verwante materiaal, wat beskikbaar is om af te laai.

Die GRN Oudiobiblioteek - Evangelistiese en basiese Bybelonderrigmateriaal wat geskik is vir die behoefte en kultuur van die mense in 'n verskeidenheid style en formate.

Choosing the audio or video format to download - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons