unfoldingWord 25 - Shetani Anamjaribu Yesu
Raamwerk: Matthew 4:1-11; Mark 1:12-13; Luke 4:1-13
Skripnommer: 1225
Taal: Swahili
Gehoor: General
Genre: Bible Stories & Teac
Doel: Evangelism; Teaching
Bybelaanhaling: Paraphrase
Status: Approved
Skrips is basiese riglyne vir vertaling en opname in ander tale. Hulle moet so nodig aangepas word dat hulle verstaanbaar en relevant is vir elke verskillende kultuur en taal. Sommige terme en konsepte wat gebruik word, het moontlik meer verduideliking nodig of selfs heeltemal vervang of weggelaat word.
Skripteks
Mara tu Yesu alipokwisha kubatizwa, Roho Mtakatifu alimwongoza Yesu nyikani, huko alifunga siku arobaini mchana na usiku. kisha Shetani alifika kumjaribu Yesu ili atende dhambi.
Shetani alimjaribu Yesu akisema; "Kama wewe ni mwana wa Mungu yaamuru mawe haya yawe mikate upate kula".
Yesu akajibu; "Imeandikwa katika neno la Mungu, watu hawahitaji mkate pekee ili wapate kuishi, bali wanahitaji kila neno linalosemwa na Mungu".
Kisha Shetani alimchukua Yesu mpaka juu ya mnara wa hekalu na kumwambia; "Kama wewe ni Mwana wa Mungu jirushe mwenyewe chini, kwa vile imeandikwa, Mungu atakuagizia malaika wake wakuchukue ili usijigonge mguu wako katika jiwe".
Lakini Yesu alimjibu Shetani kwa kunukuu Maandiko akisema; " Katika neno la Mungu, anaagiza watu wake, usimjaribu Bwana Mungu wako".
Kisha Shetani alimwonyesha Yesu falme zote za ulimwengu na fahari zake zote na akasema; "Nitakupa hivi vyote iwapo utanisujudia na kuniabudu mimi".
Yesu akajibu; ondoka kwangu Shetani! Katika neno la Mungu ameagiza, "Mwabudu Bwana Mungu wako na kumtumikia Yeye peke yake".
Yesu hakujitia chini ya majaribu ya Shetani, hivyo Shetani aliondoka akamwacha. kisha malaika walikuja na kumhudumia Yesu.