unfoldingWord 24 - Yohana Anambatiza Yesu

unfoldingWord 24 - Yohana Anambatiza Yesu

Raamwerk: Matthew 3; Mark 1; Luke 3; John 1:15-37

Skripnommer: 1224

Taal: Swahili

Gehoor: General

Genre: Bible Stories & Teac

Doel: Evangelism; Teaching

Bybelaanhaling: Paraphrase

Status: Approved

Skrips is basiese riglyne vir vertaling en opname in ander tale. Hulle moet so nodig aangepas word dat hulle verstaanbaar en relevant is vir elke verskillende kultuur en taal. Sommige terme en konsepte wat gebruik word, het moontlik meer verduideliking nodig of selfs heeltemal vervang of weggelaat word.

Skripteks

Yohana mwana wa Zakaria na Elizabeth alikuwa na akawa nabii .Aliishi nyikani akila asali ya porini, nzige ,na kuvaa nguo zilizotengenezwa na manyoya ya ngamia.

Watu wengi walimfuata Yohana nyikani kumsikiliza.Aliwahubiri akisema,"tubuni kwa maana ufalme wa Mungu umekaribia"

Wakati watu waliposikia ujumbe wa Yohana wengi walitubu dhambi zao na kubatizwa .Viongozi wengi wa dini walikuja kubatizwa na Yohana lakini hawakutubu wala kuungama dhambi zao .

Yohana akawaambia viongozi wa dini" enyi nyoka wenye sumu! tubuni na kubadilisha tabia zenu.Kila mti usiozaa matunda mema hukatwa na kutupwa motoni. Yohana alitimiza kile kilichosemwa na manabii "angalia namtuma mjumbe wangu mbele yenu ambaye atawandalia njia zenu."

Baadhi ya Wayahudi wakamwuuliza Yohana kama yeye ni Kristo ,Yohana akajibu mimi siyo Kristo lakini kuna mmoja ajaye baada yangu ambaye ni mkuu sanakwani sistahili kufungua kamba ya viatu vyake .

Siku iliyofuata Yesu alikuja ili abatizwe na Yohana .Wakati alipomwona Yohana alisema,'angalia huyu ni mwanakondoo wa Mungu atakayechukua dhambi ya ulimwengu.

Yohana akamwambia Yesu mimi sistahili kukubatiza wewe ila wewe unastahili kunibatiza mimi.Lakini Yesu akasema "ni lazima kunibatiza mimi kwa sababu ni kitu sahihi kwa hiyo Yohana akambatizaYesu pamoja na kwamba Yesu hakuwahi kutenda dhambi.

Wakati Yesu alipotoka majini baada ya kubatizwa Roho wa Mungu alitokea katika umbo la njiwa alishuka akatulia juu yake.Wakati huo sauti ya Mungu ikaongea kutoka mbinguni na kusema "Wewe ni mwanangu ambaye ninakupenda na ninayependezwa naye ".

Mungu akamwambia Yohana," Roho wa Mungu atakuja juu ya mtu ambaye umembatiza .Na mtu huyo ni mwana wa Mungu ,"Kuna Mungu mmoja tu.Lakini wakati Yohana alipokuwa akimbatiza Yesu alisikia Baba Mungu akisema na akamuona Mungu mwana ,ambaye ni Yesu ,na akamwona Roho Mtakatifu.

Verwante inligting

Woorde van Lewe - GRN het oudio-evangelieboodskappe in duisende tale wat Bybelgebaseerde boodskappe bevat oor verlossing en Christelike lewe.

Gratis aflaaie - Hier vind u al die belangrikste GRN boodskap skrips in verskeie tale, plus prente en ander verwante materiaal, wat beskikbaar is om af te laai.

Die GRN Oudiobiblioteek - Evangelistiese en basiese Bybelonderrigmateriaal wat geskik is vir die behoefte en kultuur van die mense in 'n verskeidenheid style en formate.

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the right audio or video format - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?