unfoldingWord 10 - Mapigo Kumi

unfoldingWord 10 - Mapigo Kumi

Raamwerk: Exodus 5-10

Skripnommer: 1210

Taal: Swahili

Gehoor: General

Genre: Bible Stories & Teac

Doel: Evangelism; Teaching

Bybelaanhaling: Paraphrase

Status: Approved

Skrips is basiese riglyne vir vertaling en opname in ander tale. Hulle moet so nodig aangepas word dat hulle verstaanbaar en relevant is vir elke verskillende kultuur en taal. Sommige terme en konsepte wat gebruik word, het moontlik meer verduideliking nodig of selfs heeltemal vervang of weggelaat word.

Skripteks

Watu wawili ambao ni Musa na Haruni walimwendea Farao na kumweleza kwamba, "Mungu wa Israeli anasema hivi, waruhusu watu wangu kuondoka katika nchi ya Misri." Farao hakukubali, alichofanya ni kuongeza uzito wa kazi kuliko hapo awali.

Farao aliendelea kuwakatalia Waisraeli wasiondoke, kwa sababu hiyo Mungu alileta mapigo kumi kwa Wamisri ya madhara makubwa sana. Kwa kufanya hivyo Mungu alionesha kuwa yeye anao uwezo mkubwa kuliko Farao na miungu yote ya Wamisri.

Mungu aliyabadilisha maji ya mto Naili kuwa damu. Pamoja na pigo kama hilo Farao hakutoa ruhusa kwa Waisraeli kuondoka katika nchi ya Misri.

Mungu alileta vyura kuwasumbua Wamisri wote. Farao alimwomba Musa aombe ili vyura wasiendelee kuwepo. Lakini baada ya Musa kuomba na vyura kutoweka moyo wa Farao uliendelea kuwa mgumu asiwaruhusu Waisraeli kuondoka katika nchi ya Misri.

Kwa sababu hiyo Mungu alileta pigo la chawa. Zaidi ya hapo Mungu alileta nzi, pigo ambalo lilimfanya Farao kuwaita Musa na Haruni kuwaambia kuwa kama janga hilo wataliondoa watapewa ruhusa ya kuondoka katika nchi ya Misri. Musa alimwomba Mungu kuondoa janga la nzi na Mungu akawaondoa nzi wote. Hata hivyo moyo wa Farao ulikuwa mgumu asiwaruhusu Waisraeli kuondoka.

Mungu alileta pigo la ugonjwa kwa mifugo wa Wamisri kwamba mifugo iliugua na kufa. Hata hivyo Farao alikuwa kaidi kuweza kuwaruhusu Waisreli kuondoka.

Ndipo Mungu akamwambia Musa kupeperusha majivu angani machoni pa Farao. Majivu hayo yalisababisha majipu yenye vidonda kwa Wamisri peke yake, Waisraeli hawakudhurika na majipu hayo. Mungu alimfanya Farao kuwa na moyo wa ukaidi na hivyo hakuweza kuwaruhusu Waisraeli kuondoka.

Baada ya janga la majipu, Mungu alileta mvua ya mawe iliyo haribu mazao na kuleta maafa kwa mtu yeyote aliyenyeshewa na mvua hiyo katika nchi ya Misri. Farao alionekana kujuta aliwaita Musa na Haruni na kusema, "nimefanya dhambi," sasa nitawaruhusu kuondoka. Musa alimwomba Mungu, mvua haikuendelea kunyesha.

Farao hata hivyo, hakuacha kutenda dhambi na moyo wake ukaendelea kuwa wenye ukaidi kwa kutowaachia uhuru Waisraeli kuondoka.

Kwa sababu hiyo Mungu alituma nzige wengi sana walioharibu mazao yote yaliyosalia na mvua ya mawe katika nchi ya Misri

Ndipo Mungu alileta giza totoro katika nchi ya Misri lillosababisha Wamisri wabakie majumbani mwao, wasitoke kwa muda wa siku tatu. Lakini mahali Waisraeli walipokuwa hapakuwa na giza.

Ingawa kulitokea mapigo tisa Farao hakukubali kuwaruhusu Waisraeli kuondoka. Kwa kuwa Farao hangeweza kusikiliza Mungu alikusudia kuleta pigo la mwisho. Pigo hili lingemfanya Farao kubadilisha mawazo yake.

Verwante inligting

Woorde van Lewe - GRN het oudio-evangelieboodskappe in duisende tale wat Bybelgebaseerde boodskappe bevat oor verlossing en Christelike lewe.

Gratis aflaaie - Hier vind u al die belangrikste GRN boodskap skrips in verskeie tale, plus prente en ander verwante materiaal, wat beskikbaar is om af te laai.

Die GRN Oudiobiblioteek - Evangelistiese en basiese Bybelonderrigmateriaal wat geskik is vir die behoefte en kultuur van die mense in 'n verskeidenheid style en formate.

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the right audio or video format - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?