unfoldingWord 09 - Mungu Anamwita Musa

unfoldingWord 09 - Mungu Anamwita Musa

Raamwerk: Exodus 1-4

Skripnommer: 1209

Taal: Swahili

Gehoor: General

Genre: Bible Stories & Teac

Doel: Evangelism; Teaching

Bybelaanhaling: Paraphrase

Status: Approved

Skrips is basiese riglyne vir vertaling en opname in ander tale. Hulle moet so nodig aangepas word dat hulle verstaanbaar en relevant is vir elke verskillende kultuur en taal. Sommige terme en konsepte wat gebruik word, het moontlik meer verduideliking nodig of selfs heeltemal vervang of weggelaat word.

Skripteks

Yusufu alipofariki, ndugu zake walidumu kuishi huko Misri. Wao pamoja na wazazi wao, kwa miaka mingi waliongezeka na walikuwa na watoto wengi. Kabila hilo waliitwa Waisraeli

Mamia ya miaka mingi ilipita, wakazidi kuongezeka. Wamisri walimsahau Yusufu na kazi nzuri alizozifanya kwa Wamisri. Wamisri waliwaogopa Waisraeli kwa kuwa walikuwa wengi na Farao wa kipindi hicho aliwafanya kuwa watumwa kwa Wamisri.

Waisraeli walitumikishwa na Wamisri kwa kazi ngumu kwa kujenga majumba na miji mikubwa. Ugumu wa kazi ulisababisha huzuni kimaisha. Bali baraka za Mungu ziliwazidishia watoto kwa wingi.

Farao aliona kuwa Waisraeli walikuwa wanazaa watoto wengi, aliamuru watoto wa kiume wauawe kwa kutupwa katika mto Naili.

Mtoto wa kiume alizaliwa na mama mmoja wa Kiisraeli. Wazazi wa mtoto huyo walimficha kwa muda walioweza.

Mtoto huyo alipokuwa hawezi kufichika tena, ili kumuokoa wazazi walimweka katika kikapu kieleacho na kukiweka katika majani kando ya mto Naili. Ili kujua kuwa ni jambo gani lingempata mtoto huko mtoni dada yake alikuwa akifanya uchunguzi.

Mtoto wa kike wa Farao aliona kikapu na alichungulia ndani yake. Alipoona mtoto, alimchukua awe wake na kumwajiri mwanamke wa Kiyahudi amtunze. Bila kutambua, mama huyo mlezi ndiye alikuwa mzazi wa mtoto huyo. Mtoto alipoacha kunyonya alikabidhiwa kwa binti Farao naye akamwita jina lake Musa.

Akiwa mtu mzima, siku moja Musa alimkuta Mmisri akimpiga mtumwa wa Kiisraeli. Na alijitahidi kumuokoa Mwisraeli mwenzake.

Musa alimuua Mmisri na kuuzika mwili wake akidhani kwamba hakuna mtu ambaye angemwona. Kumbe mtu mmoja alimwona akifanya kitendo hicho.

Habari za mauaji zilipomfikia Farao, aliazimia kumuua Musa. Musa alitoroka kutoka Misri na kukimbilia nyikani ili kujiokoa na walinzi wa Farao.

Musa alikuwa mchungaji wa kondoo huko nyikani mbali na nchi ya Misri. Alioa huko na kuzaa watoto wawili wa kiume.

Siku moja Musa alikuwa akichunga kondoo wake, aliona kichaka kilichowaka moto bila kuteketea. Musa alisogea kuona vizuri, alipokaribia, Mungu alisikika akisema, "Musa vua viatu vyako. Ardhi uliyosimama juu yake ni takatifu".

Mungu alimwambia Musa," Nimeyaona mateso ya watu wangu. Ili kuwakomboa kutoka utumwani huko Misri, nitakutuma wewe kwa Farao ukawaondoe Waisraeli kutoka utumwani Misri. Nami nitawapa nchi ya Kanaani, niliyowaahidia Ibrahimu, Isaka na Yakobo."

Musa akauliza, watakapotaka kujua Ni nani aliyenituma kwao nisemeje? Mungu akasema, "MIMI NIKO AMBAYE NIKO. Waambie AMBAE NIKO amenituma. Mimi ni YEHOVA Mungu wa baba zenu Ibrahimu, Isaka na Yakobo. Jina langu ndilo hilo milele."

Musa hakutaka kwenda kwa Farao kwani aliogopa, kwa sababu alihofia kutoweza kuongea vizuri. Mungu alimruhusu Haruni nduguye amsaidie. Aliwaonya kuwa Farao atakuwa na moyo mgumu.

Verwante inligting

Woorde van Lewe - GRN het oudio-evangelieboodskappe in duisende tale wat Bybelgebaseerde boodskappe bevat oor verlossing en Christelike lewe.

Gratis aflaaie - Hier vind u al die belangrikste GRN boodskap skrips in verskeie tale, plus prente en ander verwante materiaal, wat beskikbaar is om af te laai.

Die GRN Oudiobiblioteek - Evangelistiese en basiese Bybelonderrigmateriaal wat geskik is vir die behoefte en kultuur van die mense in 'n verskeidenheid style en formate.

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the right audio or video format - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?