unfoldingWord 23 - Kuzaliwa kwa Yesu

unfoldingWord 23 - Kuzaliwa kwa Yesu

Esquema: Matthew 1-2; Luke 2

Número de guión: 1223

Idioma: Swahili

Audiencia: General

Tipo: Bible Stories & Teac

Propósito: Evangelism; Teaching

Citación Biblica: Paraphrase

Estado: Approved

Los guiones son pautas básicas para la traducción y grabación a otros idiomas. Deben adaptarse según sea necesario para que sean comprendidas y relevantes para cada cultura e idioma diferentes. Algunos términos y conceptos utilizados pueden necesitar más explicación o incluso ser reemplazados o omitidos por completo.

Guión de texto

Mariamu alikuwa amechumbiwa na mtu mwadilifu aitwaye Yusufu. Yusufu kwasababu ya uhaki hakutaka Mariamu apate aibu kwaajili ya ujauzito ambao haukumhusu hivyo akaanza kutafuta njia akwepe kwa siri. Malaika akamtokea Yusufu katika ndoto.

Ndipo Malaika akamtahadharisha Yusufu kwamba asimwache Mariamu kwasababu mimba hiyo ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu hivyo asiwe na wasiwasi. Mtoto atakayezaliwa ni wa kiume ataitwa jina lake Yesu (yaani Yehova huokoa), kwa kuwa atawaokoa watu waondoke dhambini.

Yusufu aliamua kumchukua Mariamu kuwa mkewe; lakini, hawakukaribiana mpaka pale Mariamu atakapomzaa mwana.

Wakati Mariamu alipokaribia kuzaa, ni kipindi kile utawala wa Rumi ulielekeza kila mtu ahesabiwe katika jamii anayotokea. Hapa inabidi sasa Yusufu na Mariamu wasafiri safari ndefu waelekee Bethlehemu tokea Nazareti kwa sababu ndiyo mji wao kwa asali yaani mji wa Daudi.

Baada ya kufika Bethlehemu hapakuwa na mahali ya kujihifadhi. Nafasi waliyopata ni pale mifugo ilihifadhiwa, ndipo mtoto alipozaliwa na mama yake alimlaza kwenye lishio la ng'ombe kwa kuwa hakuna kitanda; jina lake aliitwa Yesu.

Usiku ule ule walikuwepo wachungaji wa maeneo jirani wakilinda mifugo yao. Ghafla waliona malaika akin'gaa mbele yao wakatekewa; Malaika akasema, "msiwe na wasiwasi ninazo habari nzuri. Kristo Bwana amezaliwa Bethlehem!"

Akaongeza; "nendeni kwa mtoto, mtamuona amefungwa nguo akiwa amelazwa kwenye lishio la mifugo." Mawinguni walionekana Malaika, wakitukuza na kuimba Utukufu uko mbinguni kwa Mungu na amani duniani kwa wapendwa."

Wachungaji walifika mahali pale alipokuwa Yesu kama maelekezo ya malaika yalivyokuwa wakiwa wamejawa furaha. Baada ya hapo wakarudi ilipokuwa mifugo yao; wakimtukuza Mungu kwa yale waliyosikia na kuyaona.

Badaye wenye ujuzi tokea mashariki ya mbali wakiongozwa na nyota walifika Bethlehemu na hapo wakatambua ile nyota ilimaanisha Mfalme wa Wayahudi. Hivyo wakasafiri safari ndefu na wakaipata nyumba alimokuwa Yesu akiwa pamoja na wazazi wake.

Na wataalamu hawa walipomuona Yesu na mama yake, wakainama na kumwabudu. Ndipo walimpa Yesu zawadi za gharama kubwa. Wakarudi kwao mashariki.

Información relacionada

Palabras de Vida - GRN tiene mensajes audios en miles de idiomas que contienen mensajes basados en la Biblia acerca de la salvación y la vida cristiana.

Descargas gratis - Aquí puede encontrar los guiones principales de GRN en varios idiomas y también imágenes y otros materiales relacionados. Todos están disponibles para descargar.

Librería de audio de GRN - Material evangelistico y de enseñanza adecuado a las necesidades y a la cultura en variedad de stilos y formatos

Copyright and Licensing - GRN shares it's audio, video and written scripts under Creative Commons

Choosing the right audio or video format - What audio and video file formats are available from GRN, and which one is best to use?